MALAIKA MIKAEL NI NANI? KULINGANA na Biblia, kuna mamilioni ya malaika wanaoishi katika makao ya kiroho. ( Danieli 7:9, 10; Ufunuo 5:11 ) Kutoka mwanzo hadi mwisho, Maandiko mara nyingi hurejezea malaika walio waaminifu kwa Mungu. Hata hivyo, ni wawili tu kati ya viumbe hao wa kiroho wanaotajwa kwa majina. Mmoja wao ni malaika Gabrieli, aliyewapelekea watu watatu tofauti-tofauti ujumbe kutoka kwa Mungu kwa kipindi cha miaka 600 hivi. (Danieli 9:20-22; Luka 1:8-19, 26-28 ) Malaika mwingine anayetajwa kwa jina katika Biblia ni Mikaeli. Bila shaka, Mikaeli ni malaika mwenye cheo cha pekee. Kwa mfano, katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anatajwa kuwa anapigana na roho waovu kwa niaba ya watu wa Yehova. (Danieli 10:13; 12:1 ) Katika barua iliyopuliziwa ya Yuda, Mikaeli amshambulia Shetani katika bishano juu ya mwili wa Musa. ( Yuda 9 ) Kitabu cha Ufunuo chaonyesha kwamba Mikaeli alipigana na Shetani na malaika zake na kuwavurumisha chini kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:7-9 ...